Uongo ni tamko lisilo kweli linalotolewa kwa makusudi. Mtu anayesema uwongo anajua au anahisi ya kwamba maneno yake si ya kweli lakini anataka msikilizaji wa maneno yake (au mpokeaji wa ujumbe wake) ayaamini kuwa kweli.
Mara nyingi uwongo hutumiwa kwa kusudi la kuficha kosa, aibu au tendo haramu. Kusudi lingine ni kujipatia faida au kuzuia hasara.
Uwongo hutazamwa kuwa tofauti na maneno yasiyo kweli lakini msemaji hajui kwamba si kweli au alikosea mwenyewe.