Upimaji

Upimaji ni kazi ya kutambua tabia za kitu kwa umakinifu. Mara nyingi tabia hizi zinatazamiwa kwa njia ya makadirio lakini kila kadirio hutegemeana na mtu mwenyewe anayekadiria. Pale ambako watu mbalimbali wanataka kulinganisha vitu viwili wakati wanatofautiana katika makadirio yao upimaji unaweza kuamua juu ya ukubwa, uzito na tabia nyingine.

Mwnazo wa vipimo ilikuwa biashara yaani tendo la kubadilishana vitu na bidhaa. Kazi hii ilihitaji vizio vya kulinganisha vitu mbalimbali.

Haiwezekani kupima kila tabia ya kitu fulani kwa mfano urembo au uzuri. Lakini tabia za kifizikia kama urefu, uzani, ujao, kasi n.k. zinapimika.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne