Victoria Falls au Maporomoko ya Viktoria (Mosi-oa-Tunya) ni maporomoko ya mto Zambezi mpakani mwa Zambia na Zimbabwe.
Mto Zambezi wenye upana wa mita 1170 unafika penye ngazi ya mwamba na maji yote yaanguka kimo cha takriban mita 110 yanapoendelea katika mfereji wa mwamba wenye upana wa m 120 pekee. Maporomoko hayo ni makubwa kabisa katika Afrika.