Visiwa vya Karibi (kwa Kiingereza Caribbean; kwa Kiholanzi: Cariben au Caraiben, kwa Kifaransa: Caraïbe au aghalabu Antilles; kwa Kihispania: Caribe) ni eneo la Amerika ambalo linajumuisha maelfu ya visiwa vikubwa na vidogo katika Bahari ya Karibi (Atlantiki), lakini pia maeneo ya kaskazini mwa Amerika Kusini na mashariki mwa Amerika ya Kati.