Vita ya Miaka Saba ilitokea kati ya miaka 1756 na 1763. Ilitokana na mashindano ya nchi za Ulaya ikasambaa pande nyingi za dunia. Hivyo imeitwa "Vita Kuu ya Dunia" ya kwanza hata kama jina hilo kwa kawaida linatumiwa kwa ajili ya vita kati ya 1914 na 1918.