Vitabu vya hekima

Miongoni mwa aina za vitabu vya Biblia vipo vile vinavyojulikana kama vitabu vya hekima.

Kati ya vitabu hivyo, Agano la Kale lina Methali , Kitabu cha Yobu, na Mhubiri, ingawa hata baadhi ya Zaburi na sehemu za vitabu vingine pia vinaweza kuhesabiwa kuwa ni maandiko ya hekima. Tena, kati ya Deuterokanoni, Kitabu cha Yoshua bin Sira na Kitabu cha Hekima ni vitabu vya hekima.

Upande wa Agano Jipya, ni hasa Waraka wa Yakobo ulioendeleza mtindo huo wa uandishi.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne