Waarusha ni kabila la watu linalopatikana kaskazini mwa Tanzania katika eneo la mlima Meru, Mkoa wa Arusha. Lugha yao ni Kiarusha inayohesabiwa kama lahaja ya Kimaasai[1]. Wakati wa kuja kwa wakoloni hao walikuwa wakazi wa eneo la mji wa Arusha wa leo.