Waarusha

Wachezaji Waarusha katika arusi wakati wa ukoloni mnamo 1936.

Waarusha ni kabila la watu linalopatikana kaskazini mwa Tanzania katika eneo la mlima Meru, Mkoa wa Arusha. Lugha yao ni Kiarusha inayohesabiwa kama lahaja ya Kimaasai[1]. Wakati wa kuja kwa wakoloni hao walikuwa wakazi wa eneo la mji wa Arusha wa leo.

  1. http://multitree.org/codes/mas-aru Kiarusha katika multitree

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne