Wakisi ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Njombe, Wilaya ya Ludewa, ukanda wa Ziwa Nyasa
Lugha yao ni Kikisi.
Jamii hiyo hujihusisha na shughuli mbalimbali zikiwemo za uvuvi, ufinyanzi, kilimo cha muhogo.
Pia ni wachezaji wazuri wa ngoma ya Mganda, Kihoda na Ligambusi.