Wakisii

Wakisii (hujulikana pia kama Abagusii au Gusii) ni kabila la Kibantu ambao hukaa katika kaunti ya Kisii na kaunti ya Nyamira, magharibi mwa Kenya.

Kisii - mji unaojulikana na wakazi wake kama Bosongo au Getembe - uko kusini magharibi mwa Kenya na ni nyumbani kwa watu wa asili ya Gusii. Jina Bosongo liliaminiwa kutokana na jina Abasongo (kwa maana ya Wazungu) ambao waliishi katika mji wakati wa ukoloni.

Mwaka 2014 walikadiriwa kuwa 3,205,669.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne