Wamakabayo

Wazao wa Matatia.
Israeli chini ya Yuda Mababayo.
Uenezi wake chini ya Yonathan Makabayo.
Uenezi wake chini ya Simoni Makabayo.

Wamakabayo (kwa Kiebrania מכבים au מקבים, Makabim au Maqabim; kwa Kigiriki Μακκαβαῖοι) walikuwa familia ya mashujaa wa Israeli walioongoza mapigano dhidi ya dola la Waseleuki ili kupata uhuru wa dini na hatimaye uhuru wa taifa upande wa siasa pia.

Mashujaa hao walikuwa kuhani Matatia na wanae watano waliopokezana kushika uongozi kuanzia Yuda Mmakabayo

Habari zao zinasimuliwa katika kitabu cha kwanza cha Wamakabayo na kitabu cha pili cha Wamakabayo vilivyoandikwa na watu tofauti katika karne II KK na ambavyo vyote viwili ni kati ya vile vya Deuterokanoni vinavyokubaliwa na Wakristo wengi kama sehemu ya Biblia. Ushujaa wao unasifiwa pia na waraka kwa Waebrania kama kielelezo cha imani.

Pia kuna vitabu vingine viwili juu yao (Wamakabayo III na Wamakabayo IV) ambavyo havimo katika toleo la Septuaginta wala katika Biblia ya Kikristo.

Ukoo wao (Wahasmonei) ulitawala Yudea tangu mwaka 164 KK hadi 63 KK, wakisisitiza dini ya Uyahudi na kupunguza athari ya ustaarabu wa Ugiriki wa kale kati ya Wayahudi.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne