Wandrili

Mt. Wandrili katika dirisha la kioo cha rangi la kanisa la Clichy.

Wandrili (pia: Wandregisel; Verdun, 605 - 22 Julai 668) alikuwa afisa katika ikulu ya mfalme Dagoberti I hadi mwaka 629 alipojifanya mmonaki chini ya Balderiki kisha kukubaliana na mke wake.

Baadaye akaishi upwekeni akaanza kufuata kanuni ya Mt. Kolumbani. Mwisho alipewa upadrisho na askofu Dado akaanzisha msituni monasteri ya aina hiyo, akaiongoza kama abati hadi kifo chake[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa kila mwaka siku ya kifo chake[2].

  1. http://www.santiebeati.it/dettaglio/92851
  2. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne