Waraka wa kwanza kwa Wathesalonike ni kitabu cha Agano Jipya katika Biblia ya Kikristo. Ni barua iliyoandikwa na Paulo wa Tarso kwa Wakristo wa mji wa Thesaloniki katika Ugiriki ya Kale.
Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.