Waziri Mkuu wa Tanzania

Waziri Mkuu wa Tanzania ni msimamizi wa shughuli zote za serikali katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Anawakilisha serikali katika bunge la taifa. Yuko chini ya mamlaka ya rais.[1] Anateuliwa na rais akihitaji kuthebitishwa na wabunge wengi.[2]

Waziri Mkuu si kiongozi wa serikali lakini anaongoza vikao vya baraza la mawaziri wakati rais na makamu wa rais hawapo.[3]

  1. Katiba ya Tanzania, fungu 52: ana "ana madaraka juu ya udhibiti, usimamiaji, utekelezaji wa siku hata siku wa kazi na shughuli za serikali; ...atakuwa Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni; ...atatekeleza au kusababisha utekelezaji wa jambo lolote au mambo yoyote ambayo Rais ataagiza "
  2. Katiba ya Tanzania, fungu 51 ""Kutakuwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano atakayeteuliwa na Rais; ...uteuzi wake uwe umethibitishwa na Bunge kwa azimio litakaloungwa mkono na kura za Wabunge walio wengi."
  3. Katiba fungu 54,2

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne