Wilaya ya Mbozi ni wilaya mojawapo kati ya 5 za Mkoa wa Songwe.
Eneo la wilaya ni kilomita za mraba 3440.
Katika sensa ya mwaka 2002, idadi ya wakazi wa wilaya hiyo ilihesabiwa kuwa 515,270. Baada ya kutenga maeneo ya wilaya mpya ya Momba na Halmashauri ya mji wa Tunduma mnamo 2012/13, Mbozi kwa mujibu wa takwimu za sensa ya watu na makazi ya 2022 ina jumla ya watu 510,599, hii ikiwa sawa na asilimia 40 ya wakazi wote wa mkoa wa Songwe ambao kwa takwimu hizo ni 1,344,687 [1]..