Wilaya ya Same

Wilaya ya Sama ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro
Mahali pa Same (kijani kilichokolea) katika mkoa wa Kilimanjaro.

Wilaya ya Same ni wilaya mojawapo kati ya wilaya 7 za Mkoa wa Kilimanjaro nchini Tanzania.

Katika sensa ya mwaka 2012, idadi ya wakazi wa wilaya hiyo ilihesabiwa kuwa 269,807. Katika ile ya mwaka 2022 walihesabiwa 300,303 [1].

Wilaya hii imepakana upande wa kazkazini na Wilaya ya Mwanga na nchi jirani ya Kenya, upande wa kusini na Mkoa wa Tanga na upande wa magharibi na Mkoa wa Manyara. Makao makuu yapo Same Mjini.

Upande wa kusini wa Milima ya Pare upo ndani ya wilaya pamoja na sehemu ya Hifadhi ya Mkomazi.[2]

Njia ya reli ya Usambara inapita wilayani.

  1. https://www.nbs.go.tz
  2. Tanzania travel guide (tol. la 6). Lonely Planet. Juni 2015. uk. 148. ISBN 978-1742207797. Iliwekwa mnamo 12 Januari 2016.{{cite book}}: CS1 maint: date auto-translated (link)

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne