Wimbisauti (au: wimbi la sauti) ni njia ya uenezaji wa sauti katika nafasi.
Kwa macho ya fizikia "sauti" ni mtetemo wa gimba (kwa mfano utando) unaoendelea kama wimbi katika midia ulipo. Kwa macho ya fiziolojia na saikolojia "sauti" ni mapokezi ya wimbisauti kwa milango ya fahamu hasa sikio na utambuzi wake katika ubongo.