Yusti na Pastori

Sanamu zao katika mnara wa kengele, Barcelona.

Yusti na Pastori (walifariki Alcalá de Henares, Hispania, 304 hivi) walikuwa wanafunzi wa shule Wakristo waliouawa kwa kukatwa kichwa katiaka dhuluma ya kaisari Dioklesyano [1]

Waliposikia gavana amefika ili kuua Wakristo, waliacha shuleni vifaa vyao vya kuandikia, wakakimbilia kifodini kwa hiari: mara walikamatwa, wakapigwa fimbo wakauawa huku wakifarijiana na kuhimizana.[2].

Inasemekana Yusti alikuwa na umri wa miaka 13, na mdogo wake Pastori chini ya miaka 9.

Mshairi Prudentius (348-410) aliwataja kwa majina.

Heshima ya watu kwao kama watakatifu wafiadini ni ya zamani sana.

Sikukuu yao huadhimishwa kila mwaka tarehe 6 Agosti[3].

  1. Saints Justus and Pastor by H.M. Magazine
  2. http://www.santiebeati.it/dettaglio/65540
  3. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne