Yves Marie Monot

Yves Marie Monot, C.S.Sp. (alizaliwa Pont-l'Abbé, Ufaransa, 29 Mei 1944) ni askofu mstaafu wa Jimbo Katoliki la Ouesso katika Jamhuri ya Kongo.

Alijiunga na Shirika la Roho Mtakatifu (Spiritans) tarehe 8 Septemba 1963 na kupadrishwa tarehe 9 Julai 1972. Baada ya upadrisho wake, aliendelea na masomo ya sayansi na theolojia katika Institut Catholique de Paris.

Baada ya Askofu Hervé Itoua kujiuzulu tarehe 22 Aprili 2006, Monot aliteuliwa kuwa msimamizi wa kitume wa Jimbo la Ouesso. Alihudumu katika nafasi hiyo hadi alipoteuliwa kuwa askofu wa Ouesso tarehe 14 Juni 2008. Alipata daraja la uaskofu tarehe 7 Septemba 2008 kupitia kuwekwa wakfu na Kardinali Ivan Dias.[1]

  1. "Rép. du Congo: Mgr Yves Marie Monot nouvel évêque de Ouesso". Catholique.org (kwa Kifaransa). 16 Juni 2008. Iliwekwa mnamo 27 Desemba 2010.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne